Monday 17 April 2017

Nape: Niliyashuhudia haya kwa miezi 38, nikiyakumbuka naonekana mkorofi.|Soma

Mbunge wa jimbo la Mtama mkoani Lindi kupitia tiketi ya CCM, Mhe. Nape Moses Nnauye ametoa ya moyoni kwa kusema kila anapokumbuka shida wanazozipata wananchi humfanya aonekane mkorofi kwa kuwa anasema ukweli.


Nape amebainisha hayo, kupitia ukurasa wake wa kijamii wa twitter huku akiwa ameambatanisha na picha ambayo inaonesha wananchi jinsi wanavyopata tabu kuvuka upande mmoja wa mto kwenda upande wa pili kwa kupita ndani ya maji hayo.

“Niliyashuhudia maisha haya mikoani kwa miezi 38, nadhani ndiyo nikiyakumbuka naonekana mkorofi !! iko haja kama Taifa kuangalia vipaumbele vyetu”. Ameandika Nape


0 comments:

Copyright © 2017 KwilasaNewsline | We Call Away| All Right Reserved|
Scroll To Top