Tuesday, 2 May 2017



Msanii Diamond Platnumz kawatumia ujumbe wasanii wenzake kwenye bongofleva kupitia ukurasa wake wa Instagram ili waweze kufanya vizuri kwenye masoko ya nje.

Ushauri wa Diamond kwa Wasaani wenzake ili waweze kufanya vizuri kwenye masoko ya nje.|Soma

Soma zaidi

Monday, 24 April 2017

Uteuzi wa Miss Tanzania namba mbili wa mwaka 2006, Jokate Mwegelo kuwa Kaimu Katibu wa Uhamasishaji wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, unaonekana kutaka kuivuruga jumuiya hiyo.

Uteuzi wa Jokate Mwegelo UVCCM Wazua Utata.|Soma

Soma zaidi

Wednesday, 19 April 2017

Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo iko katika mchakato wa kuanzisha “Mfuko wa Maendeleo ya Sanaa” ambao una dhima kubwa ya kusaidia kuinua kipato, kuongeza tija

Kutoka Bungeni: Serikali Kuanzisha Mfuko wa Maendeleo ya Sanaa ili kuwasaidia Wasanii.|Soma

Soma zaidi

Saturday, 8 April 2017

Muda mfupi baada ya Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Simon Sirro kuwaambia waandishi wa habari kuwa hawezi kusema ni lini mwanamuziki Roma na wenzake watapatikana, taarifa kutoka kwa mmiliki wa studio walipokamatiwa, amethibitisha kuwa wamepatikana.

Breaking News: Msanii Roma na wenzake waliotekwa wapatikana wakiwa Salama.|Soma

Soma zaidi

Msanii wa hip hop Roma Mkatoliki alikamatwa April 5 usiku ambapo taarifa zilianza kuenea katika mitandao ya kijamii kuwa alikamatwa studio za Tongwe Records na watu wasiojulikana akiwa na wenzake na wakapelekwa kusikojulikana.

Kamanda Sirro azungumza na Waandishi wa Habari kuhusu kutekwa kwa Msanii Roma na wenzake.|Soma

Soma zaidi

Serikali kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni, sanaa na Michezo imesema imepokea kwa mshtuko taarifa za kutoweka kwa Mwanamuziki Ibrahim Mussa kwa jina la kisanii “Roma Mkatoliki” tangu tarehe 5 Aprili 2017.

Taarifa ya Wizara ya Habari kuhusu kutekwa kwa Roma Mkatoliki.|Soma

Soma zaidi

Wednesday, 29 March 2017

Saa chache baada ya kuachiwa huru kutokana na amri ya Rais John Magufuli, Rapa Nay wa Mitego amesema kuwa atayafanyia kazi maoni ya Rais kuhusu kuboresha wimbo wake kwa namna ya pekee.

Ney wa Mitego akubali kufanyia kazi maoni Rais Magufuli kuboresha wimbo wake bila kuvuka mipaka.|soma

Soma zaidi

Sunday, 26 March 2017

Mwanamuziki Emmanuel Elibariki maarufu Nay wa Mitego (#Trueboy) amekamatwa na Polisi leo asubuhi mkoani Morogoro na kupelekwa katika Kituo cha Polisi Mvomero mkoani humo.

Nay wa Mitego amekamatwa akiwa hotelini Morogoro baada ya kuamaliza shughuli zake zilizompeleka ambapo alitakiwa kuongozana na polisi hao hadi kituo cha polisi.

“Nimekamatwa kweli. Muda Huu nikiwa hotel Morogoro baada ya kumaliza Kazi yangu iliyo ni leta. Napelekwa Mvomelo Police. Nawapenda Watanzania wote. ✊🏿✊🏿 #Truth #Wapo.” Ameandika Nay wa Mitego kupitia ukurasa wake wa Instagram.

Licha ya kuwa mwanamuziki huyo hajaeleza sababu ya kukamatwa kwake, au Jeshi la Polisi kutoa taarifa, lakini inaaminika kuwa sababu kubwa ni wimbo wake alioutoa siku za hivi karibuni unaokwenda kwa jina la Wapo.

Wimbo huo umezungumzia mambo mengi hasa ya kisiasa yanayoendelea nchini kwa sasa ikiwa ni pamoja na tuhuma zinazomkabili Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, uhuru wa vyombo vya habari na masuala ya sanaa. 

 

Nay wa Mitego (Trueboy) athibitisha kukamatwa kwake na jeshi la polisi Morogoro.|Soma

Soma zaidi

Sunday, 19 March 2017

Uongozi wa Clouds umetoa kauli nzito kuhusu Video ya Uvamizi wa Ofisi zao inayosambaa mitandaoni.

Uongozi wa Clouds umetoa kauli nzito kuhusu Video ya Uvamizi wa Ofisi zao inayosambaa mitandaoni.|Soma

Soma zaidi

Friday, 17 March 2017

Muigizaji wa Filamu Tanzania Kajala Masanja amewafungukia wanaomsema kwamba ameshindwa kumlea binti yake ‘ Paula’ na kusema anatamani awaoneshe watu hao malezi anayompatia binti yake huyo.

Kajala amewafungukia wale wanaosema eti ameshindwa kumlea binti yake Paula.|Soma

Soma zaidi

Tuesday, 14 March 2017

Mbunge wa Jimbo la Mikumi kupitia CHADEMA ambaye pia ni msanii wa 'hip hop', Joseph Haule (Profesa Jay) amesema hana kinyongo na wasanii wote waliokwenda jimboni kwake kipindi cha uchaguzi oktoba 25, 2015 kwa ajili ya kumpinga.

Profesa Jay kayaandika haya kwa wasanii walioenda Jimboni kupinga Ubunge wake mabasi kwa mabasi.|Soma

Soma zaidi


Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli amempigia simu Diamond Platnumz wakati akihojiwa Jumanne hii kwenye kipindi cha 360 cha Clouds TV.

Rais Magufuli alianza kwa kumpongeza Diamond kwa kupata mtoto wa pili akimueleza kuwa wakati wa kampeni alikuwa na mtoto mmoja.

Naye Diamond hakuchelewa kutupa ombi lake akimtaka Rais kuwasaidia wasanii wa Tanzania.

“Asante sana nimekusikia,” alisema Rais Magufuli. “Lakini nakupongeza sana kwa kuzidi kuitangaza Tanzania katika masuala ya muziki na nawapongeza wanamuziki wote hata wale wanaogiza nawapenda sana wale, Shilawadu nk, asanteni jamani.”

Rais Magufuli alivyompigia simu Diamond akiwa mubashara Clouds TV na kumpongeza.|Soma

Soma zaidi

Saturday, 11 March 2017

Msanii wa muziki wa hip hop Nay wa Mitego amefunguka kwa kumpa pole mwanadada Vanessa Mdee ambaye anashikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za kutumia na kusambaza dawa za kulevya.

Ney wa Mitego kayaandika haya kuhusu kukamatwa kwa Vanessa Mdee.|Soma

Soma zaidi

Kamishna wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Simon Siro amesema jeshi hilo bado linawashikilia Wasanii maarufu wa muziki wa kizazi kipya akiwemo Vanessa Mdee ambaye alikamatwa Jumatano na Rummy Shaeli kwa tuhuma za matumizi ya dawa za kulevya.

Akiongea na wana habari Ijumaa hii ofisini kwake kamanda amesema jeshi hilo bado linawashikilia watu hao mpaka uchunguzi utakapo kamilika.

“Juzi tulimkamata Vanesa Mdee napia tunamshikilia Rummy Shaeli taarifa zinaonyesha ni watumiaji na wasambazaji lakini upelelezi unaendelea na ukikamilika tutawafikisha mahakamani au tutamuachia. Na sio hao tu wapo wengine ambao tuna majina baadhi tumewakamata inasemekana huwa wanasafirisha dawa hizo kwenda Afrika Kusini,” amesema Siro.

Vanessa alikuwa miongoni mwa watuhumiwa wa matumizi ya dawa za kulevya waliotajwa na Mkuu mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda katika orodha yake ya pili na kuwataka kuripoti katika kituo cha kituo kikuu cha polisi. Hata hivyo Vanessa hawakuweza kufika kituoni hapo kwa wakati kwa sababu wakati agizo hilo likitolewa alikuwa nje ya nchi na kumtuma mwanasheria wake kumwakilisha.

Kamanda Siro kazungumuzia kuhusu kukamatwa kwa Vanessa Mdee na Rummy.|Soma

Soma zaidi

Wednesday, 8 March 2017

Saida Karoli

Jana kupitia kipindi cha Take One cha Clouds TV, mtangazaji Zamaradi alimuhoji mwimbaji wa muziki wa asili Saida Karoli ambapo alikiri kuwa hana haki kwenye nyimbo zake kutokana na mikataba aliyosainishwa na Meneja

Saida Karoli asimulia alivyoporwa Haki zake kisa hakujua kusoma na kuandika.|Soma

Soma zaidi


Vanessa Mdee (Vee Money)

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linamshikilia mwanamuziki Vanessa Mdee maarufu Vee Money kwa tuhuma za kujihusisha na biashara haramu ya dawa za kulevya.

Sakata la Madawa: Vanessa Mdee ajisalimisha Polisi na kupelekwa kwa Mkemia Mkuu.|Soma

Soma zaidi

Mhe.Paul Makonda (Kushoto)

Msanii wa muziki wa asili nchini Mrisho Mpoto ameamua kumkingia kifua RC Makonda ambaye kwa siku za karibuni amekuwa aki-trend kwenye mitandao ya kijamii akituhumiwa kufoji vyeti.

Mrisho Mpoto: "Angalieni utendaji wake wa kazi na siyo vyeti vyake guys,"|Soma

Soma zaidi

Thursday, 16 February 2017

Mwanamuziki Diamond Platnumz jana ameripoti Kituo Kikuu cha Polisi cha Usalama Barabarani baada ya video yake kusambaa kwenye mitandao ya kijamii ikimuonyesha akiendesha gari bila kufunga mkanda huku akiachia usukani na kucheza ndani ya gari. 

Diamond nae ajikuta mikononi mwa polisi kisa kiko hapa.|Soma

Soma zaidi

Thursday, 15 December 2016

Leo kupitia ukrasa wake wa facebook Afande Sele ametangaza rasmi kujivua uanachama wa ACT - Wazalendo kupitia andiko lake hilo Afande Sele ameandika haya....

Afande Sele kaamua kuachana na ACT - Wazalendo na kuwa raia wa kawaida.

Soma zaidi

Copyright © 2017 KwilasaNewsline | We Call Away| All Right Reserved|
Scroll To Top