Tuesday 21 February 2017

Hatimaye Mbowe anaswa na Polisi baada ya Kukaidi kujisalimisha kwa siku 13.|Soma

"Mhe. Freeman Mbowe"

Jana mchana Mwenyekiti wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Freeman Mbowe alihojiwa na Polisi kuhusu sakata la dawa za kulevya baada ya jina lake kutajwa kwenye orodha ya Makonda February 8.


Baada ya kukaa kituoni hapo kwa zaidi ya masaa mawili Waandishi wa habari waliokua nje ya eneo hilo walishuhudia Mwenyekiti huyo akichukuliwa na Gari aina ya Land Cruiser iliyofatwa na magari mengine nyuma yake na kuelekea ambako Waandishi hawakufahamu mara moja.


Baadaye msemaji wa CHADEMA Tumaini Makene alisema Polisi walienda na Mbowe kupekua nyumba zake na kuandikisha maelezo ya majirani ambapo alisema kwenye mida ya saa sita usiku wa kuamkia leo Polisi walimrudisha Mbowe kwenye kituo cha Polisi kati na wakamfungulia jalada la Uchunguzi….

0 comments:

Copyright © 2017 KwilasaNewsline | We Call Away| All Right Reserved|
Scroll To Top