Wednesday 19 October 2016

Kuelekea Mdahalo wa Tatu Leo: Wasifu wa Hillary Clinton huu hapa.

Hillary Clinton amehudumu katika nyadhifa nyingi siasa za Marekani, alikuwa mama wa taifa, seneta, waziri wa mambo ya nje. Sasa, anajaribu kwa mara ya pili kutimiza ndoto yake kuu, kuwa rais wa Marekani.

 

Mwanasiasa huyu wa Democtratic wa umri wa miaka 68 alihudumu kama waziri wa mambo ya nje wa Rais Barack Obama mwanzoni mwa utawala wake Januari 2009.

 

Alijiuzulu muda mfupi baada ya Rais Obama kuchaguliwa tena kwa muhula wa pili.

 

Ni mwanadiplomasia mashuhuri Marekani na anafahamika sana kwa kusafiri sana nchi mbalimbali na kufuata diplomasia ya kukutana ana kwa ana na wahusika.

 

Kuzoea kwake kufanya safari nyingi za kuchosha, kunamuandaa vyema kwa changamoto za safari nyingi za kampeni za urais.

 

Alijaribu mara ya kwanza kuwania urais lakini akashindwa na Rais Obama wakati wa mchujo wa chama cha Democratic mwaka 2008.

 

Hillary Rodham Clinton

 

  • Alizaliwa 26 Oktoba, 1947 mjini Chicago

     

  • Alihitimu kutoka Chuo Kikuu cha Sheria cha Yale, 1973

     

  • Aliolewa na Bill Clinton mwaka 1975

     

  • 1993-2001: Alipigania kupanuliwa kwa bima ya afya na haki za wanawake alipokuwa mama wa taifa

     

  • Alichaguliwa seneta wa New York mwaka 2000

     

  • Alichaguliwa tena kwa kura nyingi 2006

     

  • 2008: Alishindwa mchujo wa kuteua mgombea urais chama cha Democratic

     

  • 2009-2013: Alihudumu kama Waziri wa mambo ya nje

     

    Chanzo cha Habari: BBC

0 comments:

Copyright © 2017 KwilasaNewsline | We Call Away| All Right Reserved|
Scroll To Top