Thursday 6 October 2016

Wasichana wa Tanzania kujadiliana na Michelle Obama

Wasichana 25 wa Tanzania wanatarajiwa kufanya majadiliano ya moja kwa moja na mke wa Rais wa Marekani, Bi Michelle Obama wiki ijayo.

 Wasichana hao ni miongoni mwa wasichana wa nchi tatu watakaoshiriki majadiliano hayo yenye lengo la kumuwezesha mtoto msichana katika masuala mbalimbali na upatikanaji wa fursa na kuzungumuzia hali ya ukatili wa kijinsia nchini Tanzania. Nchi zingine ni Peru na Cambodia.

 Majadiliano hayo ni tukio litakalofanywa na Shirika la Plan International Tanzania na yatafanyikia katika ubalozi wa Marekani, wakati wa maadhimisho ya Siku ya Msichana Duniani tarehe 11 Oktoba, 2016.

Chanzao BBC.


0 comments:

Copyright © 2017 KwilasaNewsline | We Call Away| All Right Reserved|
Scroll To Top